Katibu Muhtasi Chama cha Walimu Tanzania(CWT) Tanzania
Job Type: Full-Time
Closing Date: 1st September 2026
Location: Tanzania

Chama cha Walimu Tanzania (CWT) - Nafasi ya Kazi

Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ni Chama cha Wafanyakazi kutoka kada ya Walimu, chenye shughuli zake Tanzania Bara. Kimesajiliwa chini ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Namba 6 ya mwaka 2004 na kinaajiri Wafanyakazi kwa ajira ya kudumu katika Mikoa, Wilaya na Makao Makuu.

Ili kuboresha huduma kwa wanachama, CWT kinatangaza nafasi za ajira kwa Mtanzania yeyote mwenye sifa kwa ajili ya nafasi ya Katibu Muhtasi na Mwanasheria, atakayekuwa tayari kufanya kazi mahala popote nchini Tanzania.

1. KATIBU MUHTASI - NAFASI 27

Sifa za Waombaji:

Majukumu ya Kazi:

Masharti ya Jumla:

  1. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45.

  2. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.

  3. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya Wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.

  4. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala.

  5. Cheti cha mtihani wa Kidato cha IV na VI.

  6. Vyeti vya kitaaluma.

  7. Waombaji wawe na uzoefu usiopungua miaka miwili.

  8. Picha moja passport size ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.

  9. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA).

  10. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

  11. Maombi yanaweza kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili au Kiingereza.

  12. Waombaji watakaokidhi vigezo ndiyo watakaoitwa kwenye usaili.

  13. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 01 Septemba, 2026 saa 10:00 jioni kupitia anwani ifuatayo:

Katibu Mkuu,
Chama cha Walimu Tanzania,
S.L.P. 3077,
DODOMA.

Barua pepe: info@ttu.or.tz