Bodi ya chama cha ushirika wa akiba na mikopo Lulu(Lulu Saccos Ltd) MBR.737 kilichopo Jiji la Mbeaya maeneo ya Soweto kata ya Ruanda kinatoa tangazo la kazi kwa nafasi zifuatazo:-
Mhasibu Msaidizi - Nafasi 1
Sifa
- Awe na umri kuanzia 23 hadi 40
- Awe na elimu ya sekondari
- Awe na stashahada ya uhasibu na ushirika
- Awe ni mtanzania anayeishi katika Jiji la Mbeya
- Awe hajawahi kufukuwa kazi mahala popote kwa kosa la jinai
- Awe mtu wa kujituma
- Awe anajua kutumia kompyuta
- Awe mtu anayejisimamia mwenyewe
- Awe ni mzaliwa/mwenyeji wa mkoa wa Mbeya
Kazi
- Kusimamia na kuratibu shuguli zote za makarani wa fedha
- Kuandika na kutunza vitabu na kumbukumbu nyingine za fedha
- Kupokea malinganisho ya hesabu ya benki ya kila siku
- Kuandaa taarifa ya fedha ya kila mwezi
- Kufunga vitabu vya hesabu za chama na kuziwasilisha kwa mhasibu wa chama
- Atawajibika kwa mhasibu wa chama
- Kufanya kazi zingine atakazopangiwa na mwajiri wake
- Kazi hii ni ya mkataba wa miaka miwili
Utaratibu wa kuomba
- Mwombaji anatakiwa kuambatanisha picha mbili passport size
- Mwombaji atatakiwa kuambatanisha vivuli vya vyeti vya kuzaliwa na vya masomo
- Mwombaji aambatanishe CV yake wakati wa kuomba kazi
- Mwombaji aonyeshe mawasiliano yake bayana
- Mwombaji atakayefaulu kwa awamu ya kwanza ataitwa kwenye usaili
- Mwombaji atakeyeitwa kwenye usaili aje na vyeti halisi siku ya usaili
- Mwombaji atajigharamia mwenyewe wakati wa usaili
- Maombi yatumwe kwa:-
MWENYEKITI WA BODI
CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO LULU
S.L.P 3467
MBEYA