Analyze your CV for Mhasibu Msaidizi at Lulu Saccos Ltd

Get a free, instant analysis of how well your CV matches this role. Identify ATS issues, keyword gaps, and actionable improvements to boost your chances.

About this job

Bodi ya chama cha ushirika wa akiba na mikopo Lulu(Lulu Saccos Ltd) MBR.737 kilichopo Jiji la Mbeaya maeneo ya Soweto kata ya Ruanda kinatoa tangazo la kazi kwa nafasi zifuatazo:-
Mhasibu Msaidizi - Nafasi 1
Sifa

Awe na umri kuanzia 23 hadi 40
Awe na elimu ya sekondari
Awe na stashahada ya uhasibu na ushirika
Awe ni mtanzania anayeishi katika Jiji la Mbeya
Awe hajawahi kufukuwa kazi mahala popote kwa kosa la jinai
Awe mtu wa kujituma
Awe anajua kutumia kompyuta
Awe mtu anayejisimamia mwenyewe
Awe ni mzaliwa/mwenyeji wa mkoa wa Mbeya

Kazi

Kusimamia na kuratibu shuguli zote za makarani wa fedha
Kuandika na kutunza vitabu na kumbukumbu nyingine za fedha
Kupokea malinganisho ya hesabu ya benki ya kila siku
Kuandaa taarifa ya fedha ya kila mwezi
Kufunga vitabu vya hesabu za chama na kuziwasilisha kwa mhasibu wa chama
Atawajibika kwa mhasibu wa chama
Kufanya kazi zingine atakazopangiwa na mwajiri wake
Kazi hii ni ya mkataba wa miaka miwili

Utaratibu wa kuomba

Mwombaji anatakiwa kuambatanisha picha mbili passport size
Mwombaji atatakiwa kuambatanisha vivuli vya vyeti vya kuzaliwa na vya masomo
Mwombaji aambatanishe CV yake wakati wa kuomba kazi
Mwombaji aonyeshe mawasiliano yake bayana
Mwombaji atakayefaulu kwa awamu ya kwanza ataitwa kwenye usaili
Mwombaji atakeyeitwa kwenye usaili aje na vyeti halisi siku ya usaili
Mwombaji atajigharamia mwenyewe wakati wa usaili
Maombi yatumwe kwa:-

MWENYEKITI WA BODI
CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO LULU
S.L.P 3467
MBEYA