Wakala wa Huduma ya Faiba Tanzania Telecommunication Company Limited (TTCL) Tanzania
Full-Time
16th December 2025

FURSA YA KAZI

WAKALA WA USAJILI HUDUMA YA FAIBA

TTCL Corporation

Shirika la Mawasiliano Tanzania - TTCL Corporation linakaribisha vijana wenye uwezo kwa ajili ya kazi ya Uwakala wa usajili wa wateja wa Faiba katika jiji la Dar es salaam.

1. SIFA ZA WAOMBAJI

  • Umri usiopungua miaka 18.

  • Awe raia wa Tanzania mwenye kitambulisho halali kimoja au zaidi kati ya vifuatavyo; Kitambulisho cha Taifa (NIDA), Kitambulisho cha Mpiga Kura,leseni ya Udereva, au kitambulisho kingine kinachotambulika kisheria.

  • Awe na cheti cha kuhitimu Kidato cha Nne.

  • Awe anaishi Dar es salaam.

  • Awe na uwezo wa kusoma na kuandika Kiswahil na /au Kiingereza.

  • Awe na nidhamu, uadilifu, na asiwe na rekodi ya makosa yoyote ya jinai au mashtaka yanayohusiana na uaminifu.

  • Awe na uwezo wa kutumia simu janja (smartphone) kwa shughuli za kijidigitali.

  • Awe tayari kupokea mafunzo na kufuata taratibu za Shirika.

  • Awe na uwezo wa kujieleza na kuwasiliana na wateja.

2. TARATIBU ZA MAOMBI

  • Waombaji wote wafike TTCL Kijitonyama, wilaya ya Kinondoni, Dar es salaam tarehe 16/12/2025 kuanzia saa 03:00 asubuhi kwa ajili ya usahili wakiwa na viambatanishi elekezi.

Kwa taarifa zaidi tafadhali wasiliana nasi kupitia 0222 100 100 au barua pepe: dg@ttcl.co.tz

Application
Login to Quickly Apply