Analyze your CV for Dereva at The School of St Judes

Get a free, instant analysis of how well your CV matches this role. Identify ATS issues, keyword gaps, and actionable improvements to boost your chances.

About this job

Tangazo la Kazi: Nafasi za Udereva (1) 
  
Kuhusu Shule
Shule ya St Jude ni shule inayotoa elimu ya hisani ndani ya Tanzania. St Jude’s inafadhiliwa na wafuasi wa ukarimu kutoka kote ulimwenguni ambao hufanya dhamira yetu ya kuwapa wanafunzi wa Kitanzania mahiri na wanaotoka kwenye mazingira ya kimaskini elimu bure na yenye ubora. 
 
Shule ya St.Jude inayofuraha kutangaza nafasi Moja (1) ya kazi ya Udereva kwa watanzania wenye sifa stahiki. 
 
Kazi na Majukumu  

Kuendesha magari ya shule kwa uangalifu na umakini 


Kuwa makini na kukagua  mara kwa mara gari ulilokabidihiwa kuhakikisha lipo salama kabla ya na wakati wa kuliendesha 


Kutunza taarifa za gari/vipuri/mafuta na mabadiliko yoyote ikiwemo kujaza “log book” kwa usahihi na kwa kila tukio na safari za gari 


Kuripoti kwa wakati muda wa gari kukarabatiwa na/au kwenda “service” 


Kufuata taratibu sheria kanuni na miongozo ya usalama barabarani 


Kutoa ushirikiano kwa mamlaka ya shule na taasisi husika pale linapotokea tatizo kwa gari la shule unaloendesha 


Kufuata mipangilio na ratiba za magari na maelekezo ya Dereva Mkuu kuhusu Route za magari 


Kushiriki sikukuu na shughuli za kijamii za The School of St. Jude mara zipangwapo 


Kutoa taarifa ya maandishi ikiwa gari unaloendesha litapata hitilafu au ajali itakayozuia safari iliyopangwa au ruti kuendelea. 

 
Sifa za Mwombaji 

Awe Mtanzania mwenye umri usiopungua miaka 35. 


Ajue kusoma na kuandika vizuri kwa Kiswahili. Kuzungumza, kuandika na/au kusoma kiingereza itaboresha ombi. 


Awe na leseni hai ya udereva ya daraja “C-plain” 


 Cheti cha Udereva kutoka kwenye chuo kinachotambulika 


Awe na uzoefu wa angalau miaka miwili (2) kuendesha mabasi   ya shule.  

 
Vigezo na Masharti 
Mwombaji anatakiwa kutimiza masharti yafuatayo kikamilifu 

Barua ya maombi iambatanishwe na; 


Wasifu binafsi (CV)  


Barua ya uhakiki wa leseni kutoka polisi. 


Nakala ya cheti cha kuzaliwa 


Barua ya utambulisho kutoka kwa Mwenyekiti wa Mtaa anapoishi 


Kuambatanisha cheti/nyaraka za kughushi itapelekea kuchukuliwa hatua za kisheria 


Maombi yawasilishwe katika Shule ya St. Jude Kampasi ya Moshono kabla au jumatatu, tarehe 28 Aprili 2025. Maombi yatakayowasilishwa baada ya tarehe na muda uliopangwa hayatafanyiwa kazi.  

 
TUTAWASILIANA NA WALE TU WATAKAOKIDHI VIGEZO NA SIFA KWA AJILI YA MAJARIBIO NA MAHOJIANO! 
 
 
ANGALIZO: 
TAFADHALI KUWA MAKINI NA MATENDO YA UDANGANYIFU KATIKA MATANGAZO YA KAZI NA MCHAKATO WA AJIRA. SHULE YA ST JUDE HAIOMBI MALIPO KATIKA HATUA YOYOTE YA MCHAKATO WA KUAJIRI. MAOMBI YOYOTE YA MALIPO YAKATALIWE NA KURIPOTIWA KWA MAMLAKA YA UTEKELEZAJI WA SHERIA ZA MITAA KWA HATUA STAHIKI.