Analyze your CV for Mfanya Usafi at The School of St Judes

Get a free, instant analysis of how well your CV matches this role. Identify ATS issues, keyword gaps, and actionable improvements to boost your chances.

About this job

Tangazo la Kazi: Mfanya Usafi (Kampasi ya Sisia, Moshono, Arusha)

Kuhusu St Jude
Shule ya St Jude ni shule inayotoa elimu ya hisani ndani ya Tanzania. St Jude's inafadhiliwa na wafuasi wa ukarimu kutoka kote ulimwenguni ambao hufanya dhamira yetu ya kuwapa wanafunzi wa Kitanzania mahiri na wanaotoka kwenye mazingira ya kimaskini elimu bure na yenye ubora.

Shule ya St. Jude inayofuraha kutangaza nafasi ya kazi ya mfanya usafi kwa watanzania wenye sifa stahiki.

Kazi na Majukumu:

Fanya usafi wa samani (fanicha) vifaa, vyumba na maeneo ya jumuiya kama kumbi na mabwalo.
Safisha na hakikisha unamwaga dawa ya kuuwa vijidudu maliwato na jikoni.
Dumisha usafi wa vifaa na viwe katika hali nzuri.
Fanya kazi nyingine kama utakavyo agizwa na Mwajiri au mwakilishi wa Mwajiri.
Na kazi nyingine yoyote utatakayo pangiwa na kiongozi wako wa kazi kwa muda wowote.
Kuhakikisha kwamba Vyombo vya Chakula havizagai ovyo hovyo.
Kuweka kumbukumbu ya Vifaa vya Usafi vinavyotumika ili kusaidia kupanga Bajeti.
Hakikisha unajaza na kuwasilisha fomu za usafi kwa wakati kwa Makamu Mkuu wa Shule Operesheni.


Sifa za Mwombaji:

Mwombaji anatakiwa awe mkazi wa Moshono, hasa hasa jirani na shule ya St. Jude kampasi ya Sisia.
Mwombaji awe na uzoefu wa kufanya usafi kwenye mazingira ya shule.
Mwombaji awe anaishi mazingira ya karibu na shule ya St Jude kampasi ya Sisia Moshono Arusha.
Mwombaji awe Mtanzania mwenye Umri usio pungua miaka 28.
Mwombaji awe na ujuzi wa kuwakarimu watu na kufwata taratibu za kazi.


Vigezo na Masharti:
Mwombaji anatakiwa kutimiza masharti yafuatayo kikamilifu:

Mwombaji anatakiwa awe mkazi wa Moshono, hasa hasa jirani na shule ya St. Jude kampasi ya Sisia.
Aambatanishe barua ya maombi na Maelezo binafsi (CV).


Jinsi ya Kuomba:
Maombi yawasilishwe katika Shule ya St. Jude Moshono Kampasi ya Sisia kabla au mnamo Ijumaa, tarehe 3 Julai 2026. Maombi yatakayowasilishwa baada ya tarehe na muda uliopangwa hayatafanyiwa kazi.

TUTAWASILIANA NA WALE WATAKAOKIDHI VIGEZO NA SIFA KWA AJILI YA MAHOJIANO!

ANGALIZO:
TAFADHALI KUWA MAKINI NA MATENDO YA UDANGANYIFU KATIKA MATANGAZO YA KAZI NA MCHAKATO WA AJIRA. SHULE YA ST JUDE HAIOMBI MALIPO KATIKA HATUA YOYOTE YA MCHAKATO WA KUAJIRI. MAOMBI YOYOTE YA MALIPO YAKATALIWE NA KURIPOTIWA KWA MAMLAKA YA UTEKELEZAJI WA SHERIA ZA MITAA KWA HATUA STAHIKI.