Katibu Muhtasi
Job Description
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) - Nafasi ya Kazi
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ni Chama cha Wafanyakazi kutoka kada ya Walimu, chenye shughuli zake Tanzania Bara. Kimesajiliwa chini ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Namba 6 ya mwaka 2004 na kinaajiri Wafanyakazi kwa ajira ya kudumu katika Mikoa, Wilaya na Makao Makuu.
Ili kuboresha huduma kwa wanachama, CWT kinatangaza nafasi za ajira kwa Mtanzania yeyote mwenye sifa kwa ajili ya nafasi ya Katibu Muhtasi na Mwanasheria, atakayekuwa tayari kufanya kazi mahala popote nchini Tanzania.
1. KATIBU MUHTASI - NAFASI 27
Sifa za Waombaji:
Mwombaji anatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:
Awe amehitimu kidato cha nne au zaidi.
Awe na Cheti ngazi ya NTA Level 4, 5 na 6 ya Uhazili inayotambuliwa na NACTE.
Awe na uzoefu wa kutumia kompyuta na matumizi ya intaneti.
Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili.
Awe na uwezo wa kutumia lugha ya Kiswahili na Kiingereza kwa ufasaha.
Majukumu ya Kazi:
Kusimamia kesi mbalimbali za Chama na Wanachama katika Mahakama na Taasisi zenye mamlaka ya kusikiliza mashauri.
Kusoma na kutafsiri Sheria na maandiko mbalimbali ya kisheria.
Kutoa ushauri wa Kisheria kwa Walimu na Chama.
Kutatua migogoro ya kikazi wanayokabiliana nayo Walimu.
Kufuatilia utekelezaji wa changamoto mbalimbali za Walimu katika ofisi za Serikali na Waajiri.
ajira
Masharti ya Jumla:
Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45.
Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya Wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala.
Cheti cha mtihani wa Kidato cha IV na VI.
Vyeti vya kitaaluma.
Waombaji wawe na uzoefu usiopungua miaka miwili.
Picha moja passport size ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA).
Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
Maombi yanaweza kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili au Kiingereza.
Waombaji watakaokidhi vigezo ndiyo watakaoitwa kwenye usaili.
Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 01 Septemba, 2026 saa 10:00 jioni kupitia anwani ifuatayo:
Katibu Mkuu,
Chama cha Walimu Tanzania,
S.L.P. 3077,
DODOMA.
Barua pepe: info@ttu.or.tz